MBETO: NENDENI BUNGENI MKASIMAMIE MASLAHI YA ZANZIBAŔ
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar WAJUMBE watano kutoka Baraza la Wawakilishi walioteuliwa kuiwakilisha Zanzibar katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wametakiwa wakayasimamie maslahi ya Zanzibar kwa mujibu wa katiba na makubaliano ya Muungano ya mwaka 1964. Akizungumza katika kipindi cha Safari ya Bahari kinachorushwa na Bahari FM , mjini Unguja, Zanzibar 28 Januari 2026 Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar, Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo Khamis Mbeto Khamis alisema Wajumbe hao kutoka Baraza la Wawakilishi ambao wameenda kuwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano watambue wajibu wao kuwa ni kuitetea Zanzibar na sio wameenda huko kukaa kimya. "Wakajenge hoja za nguvu na sio nguvu za hoja kuhusiana na mgawanyiko wa raslimali za Taifa ikiwemo mikopo na misaada inayokuja kwa jina la Muungano wa Tanzania na pia sua...