Na Mwandishi Wetu, Zanzibar Awamu ya nane chini ya Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar na mgombea tena nafasi hiyo katika uchaguzi mkuu ujao 29 Oktoba 2025, ndio serikali pekee Afrika ambako wazee wote waliofikisha umri wa miaka 70 wanalipwa posho bila kujali iwapo ana pensheni ya kustaafu au la. Akizungumza na wanahabari, Katibu wa Kamati Maalum ya NEC, Zanzibar Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Khamis Mbeto Khamis alisema kwenye masuala ya ustawi wa jamii, Rais Dkt. Mwinyi amefanya mambo makubwa kuliko kiongozi yoyote, Afrika. Alisema awali waliofikisha miaka 70 waliopo mitaani na katika nyumba za kutunzia wazee wanalipwa TSh.40,000 kila mwezi na pesa hizo ni tofauti na TSh.50,000 ya pensheni kwa wastaafu ambayo awali ilikuwa TSh.20,000. "Ukikuta mtu huyo alikuwa mtumishi wa umma na sasa kastaafu anakula 90,000 kwa mwezi" alisema Mbeto. Alibainisha kuwa mzee kama huyo kama anayeishi nyumba za kulelea wazee za Sebuleni, L...