MKUTANO WA AFYA NORDIC, AFRIKA LEO STOCKHOLM
Na Mwandishi Wetu, Stockholm Sweden
Uzinduzi wa Mkutano wa Ngazi ya Juu wa Afya kati ya nchi za Afrika na Nordic (African–Nordic Health Summit, unafanyika leo 22 January 2026, Jijini Stockholm nchini Sweden, Tanzania ikiwakilishwa na Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Florence Samizi.
Naibu huyo Waziri ambaye ameenda kwa niaba ya Waziri wa Afya, Mohamed Omary Mchengerwa na amepokewa Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Sweden na Balozi, Mobhare Matinyi 21 Januari 2026.
Mkutano huo ambao umeandaliwa kwa ushirikiano kati ya kundi la Mabalozi wa Afrika wanawake wa nchi za Nordic, The Maternity Foundation, Dalberg Media na Danish Alliance for Global Health, pamoja na wadau wengine wa kimataifa akiwemo Global Financing Facility, World Diabetes Foundation, Ferring Pharmaceuticals na Laerdal Global Health, lengo kuu ni kujadili masuala ya afya ya uzazi na mtoto.




Comments
Post a Comment