Posts

Showing posts from February, 2026

WAZIRI DKT. KIJAJI UWANDANI KUDHIBITI TEMBO

Image
KUELEKEA siku ya Wanyamapori Duniani,  Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, yuko uwandani katika Pori la Akiba Mkungunero kuyafunga makindi ya Tembo Visukuma mawembi ili kufahamu muelekeo wao, kwa lengo la kuwazuia kuleta madhara kwa wananchi na mazao yao.  Zoezi hili pia ni utekelezaji wa maelekezo ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Lameki Nchemba ya kuwadhibiti Wanyamapori wakali na waharibifu husani Tembo.

PROFESA JANABI AZINDUA WODI YA WATOTO WACHANGA KWIMBA

Image
 Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi, akimuwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus, amezindua  jengo maalum la kisasa la kuhudumia watoto wachanga hususan wanaozaliwa kabla ya wakati (njiti) katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza Februari 28, 2026, hatua inayolenga kuinua huduma za afya ya mama na mtoto katika mkoa huo.                       Jengo hilo limejengwa kwa ufadhili wa Doris Mollel Foundation (DMF) kwa kushirikiana na Keep a Child Alive (KCA), likiwa na lengo la kupunguza vifo vya watoto wachanga na kuboresha mazingira ya utoaji huduma kwa watoto njiti, sambamba na kuunga mkono juhudi za serikali katika kuimarisha sekta ya afya. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi, Prof. Janabi amesema uwekezaji huo unaonyesha dhamira ya dhati ya wadau wa maendeleo katika kuhakikisha watoto wanaozaliwa kabla ya wakati wanapata huduma bor...

DKT MWINYI: MASHINDANO QURAAN YANAITANGAZA NCHI KIMATAIFA

Image
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi leo, t28 Februari 2026, amehudhuria fainali ya Mashindano ya 22 ya Kimataifa ya Quraan Tajweed yaliyoandaliwa na Taasisi ya Khidmatul Quran Tanzania katika Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC), jijini Dar es Salaam, yakihusisha washiriki kutoka Mataifa 12 Duniani. Rais Dkt. Mwinyi ameeleza kuwa mashindano hayo ni jukwaa muhimu la kuimarisha mapenzi ya Quraan, kukuza vipaji vya vijana na kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia taaluma ya usomaji wa Quraan.  Usomaji wa Quraan kwa kuzingatia kanuni za Tajweed si tu taaluma, bali ni msingi wa kujenga kizazi chenye maadili mema, nidhamu ya kiroho na hofu ya Mwenyezi Mungu. Ameipongeza Taasisi ya Khidmatul Quran kwa kuendeleza mashindano haya kwa kiwango cha kimataifa, jambo linaloipa nchi yetu heshima na hadhi kubwa. Vilevile, amewapongeza washiriki wote kwa ustadi wao wa hali ya juu na kuwashukuru wadhamini, hususan Benki ya CRDB kupitia kitengo...

WAZIRI KAIRUKI ATAJA MAMBO MATATU SEKTA MAWASILIANO

Image
                                    Na Mwandishi Wetu, Dodoma WAZIRI wa Sayansi na Teknolojia ya Habari, Angellah Jasmine Mbelwa  Kairuki ametaka utendaji wenye weledi, maadili na ubora wa huduma katika kudumisha misingi na maendeleo ya sekta ya mawasiliano nchini. Akizungumza wakati wa mkutano wa kikao kazi baina ya wizara, bodi na taasisi zilizo chini ya wizara hiyo, Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma 27 Februari 2026 aliiwataka menejimenti na bodi kuhakikisha kunakuwa na uwajibikaji, weledi, uwazi na uadilifu katika utendaji wa kazi ili wananchi wapate huduma bora na zenye tija. Waziri Kairuki ametaka misingi imara ya maendeleo inajengwa, uongozi thabiti na usimamizi bora wa raslimali za umma. Pia amewataka watendaji hao kuongeza kasi ya uwekezaji na uboreshaji wa miundombinu hususan kwenye maeneo yasiyo na huduma muhimu ili kuinua wigo wa upatikanaji wa huduma za mawasiliano ili kupunguza peng...

TUME, MUFTI WATETA MATUKIO 29 OKTOBA 2025

Image
TUME ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyojitokeza wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, leo Februari 27, 2026 imekutana na  Sheikh Mkuu wa Baraza Kuu la Waislam (BAKWATA), Mufti Sheikh, Alhaj Abubakar Zubeir.  Mkutano huo wa Tume na Mufti umefanyika katika Ukumbi wa Lake Tanganyika uliopo Jengo la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Jijini hapa. Miongoni mwa yaliyojadiliwa ni pamoja na namna matukio hayo yalivyoanza, athari zake kwa watu, mali na miundombinu pia ushauri wa namna ya kuondokana na matukio hayo. Hivi karibuni Mamlaka ya Uteuzi imeiongezea Tume muda wa siku arobaini na mbili (42) kuanzia tarehe 20 Februari, 2026 ili Tume iweze kukamilisha uchunguzi wa matukio hayo ambapo imetakiwa ikamilishe kazi na kuwasilisha Taarifa yake kabla au ifikapo tarehe 3 Aprili, 2026.  Kwa sasa Tume inaendelea na mahojiano na watu mbalimbali wakiwemo waathirika wa Matukio hayo.

BALOZI DKT. NCHIMBI: MASHUJAA WA MAJIMAJI WAENZIWE KWA MAMBO MATATU

Image
                               Na Ofisi ya Makamu wa Rais Songea, Ruvuma. MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amesema Mashujaa wa Vita ya Majimaji wanapaswa kuenziwa kwa kuimarisha nidhamu ya utendaji kazi, kupinga masuala ya ukabila na kutambua wajibu wa pekee wa kulitetea na kulipigania Taifa. Makamu wa Rais amesema hayo, wakati wa kilele cha Tamasha la 17 la Kumbukizi ya Miaka 120 ya Mashujaa wa Vita ya Majimaji, lililofanyika katika Viwanja vya Makumbusho ya Vita ya Majimaji, Songea mkoani Ruvuma leo 27 Februari 2026.                           Amesema ni muhimu kuwaenzi mashujaa hao kwa kuendelea kusimamia umoja ili kuhakikisha makabila yote yanakuwa Taifa moja, kufanya kazi kwa bidii kuijenga Nchi, pamoja na kupinga vitendo vya rushwa na kutenda haki.  Ameongeza kwamba, Mashujaa wa Vita ya ...

DKT. MWINYI: WAWEKEZAJI WA UFARANSA KARIBUNI ZANZIBAR

Image
 LEO 27 Februari 2026, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi amekutana na Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Bi. Anne Sophie, Ikulu Zanzibar, kwa mazungumzo yaliyolenga kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano kati ya Zanzibar na Ufaransa. Katika mazungumzo hayo, Rais Mwinyi amekaribisha makampuni na wawekezaji kutoka Ufaransa kuja kuwekeza Zanzibar, hususan katika sekta za kimkakati kama utalii, uchumi wa buluu, afya, elimu, na maendeleo ya miundombinu. "Zanzibar iko tayari kupokea uwekezaji wenye tija, unaozingatia ubora, uendelevu na maslahi mapana ya wananchi wetu. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea kuimarisha mazingira bora ya uwekezaji kwa kuboresha sera, sheria na miundombinu, ikiwemo ujenzi wa Bandari Jumuishi ya Mangapwani, pamoja na mkakati maalum wa kukiendeleza Kisiwa cha Pemba kuwa kitovu cha utalii na uwekezaji endelevu" anasema. Amewahakikishia washirika wetu wa Ufaransa kuwa Zanzibar itaendelea kuimarisha dip...

CCM: TUNAAMINI KATIKA SERIKALI YA MUUNDO WA KITAIFA ZANZIBAR

Image
                                      Na Mwandishi Wetu, Zanzibar CHAMA cha Mapinduzi (CCM) kinaamini mfumo wa Serikali ya Umoja wa kiTaifa ndio mfumo bora na salama wa kiutawala, Zanzibar. Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar, Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo Khamis Mbeto Khamis akizungumza Mjimi Unguja 27 Februari 2026 alisema kuwa wananchi wanatarajia vyama vilivyopata kura nyingi vitasaidiana kuunda serikali kwa maslahi mapana ya nchi. Alisema hayawezi kupuuzwa matakwa ya sehemu moja ya nchi akirejea chaguzi zilizopita ambapo takribani viti vya Uwakilishi Pemba vilichukuliwa na CUF enzi hizo na CCM kushinda vya Unguja. "Pemba viti vyote vilikuwa CUF enzi hizo na matokeo yalikuwa kwa asilimia 51 kwa 49 na ACT kwa asilimia zao 23 za sasa huwezi kuwapuuza" alisema Mbeto. Alibainisha kuwa kwa misingi hiyo CCM ndio maana inaendeleza utamaduni wa mazungumzo na maridhiano kwa ajili ya ustaw...

DKT. MAGEMBE: HAKUNA MGONJWA WA KIPINDUPINDU, CHUKUENI TAHADHARI

Image
                                     Na Hassan Kimweri, WAF - Morogoro Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Grace Magembe amewataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha ili kujikinga na magonjwa ya mlipuko. Amewataka wananchi kuepuka uchafuzi wa mazingira, kuwa na matumizi sahihi ya maji safi na salama na unawaji wa mikono.  Dkt. Magembe ametoa rai hiyo Februari 25, 2026 katika tamko alilolitoa la mwenendo wa magonjwa ya mlipuko na udhibiti wa kipindipindu nchini na takriban mwezi mmoja sasa hakujatokea  mgonjwa wa kipindupindu.  "Serikali imejipanga kufuatilia na kutoa huduma dhidi ya magonjwa yote ya mlipuko na itaendelea kutoa taarifa mara kwa mara iwapo kutakuwa na mabadiliko katika mwenendo wa maambukizi au endapo kutahitajika kuchukua hatua zaidi," amesema Dkt. Magembe.

KAIMU WAZIRI BIASHARA AKAGUA MWENENDO WA BEI MASOKO, UNGUJA

Image
                                            Na Mwandishi Wetu, Zanzibar KAIMU Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Sharrif Ali Sharrif, leo 25 Februari 2026 amefanya ziara katika masoko mbalimbali Unguja kukagua utekelezaji wa bei elekezi kwa bidhaa za vyakula uliotolewa na Serikali katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.                            Katika ziara hiyo alizungumza na wafanyabiashara kupata mrejesho wa moja kwa moja kuhusu upatikanaji na bei za bidhaa muhimu Anasema wafanyabiashara wameonyesha ushirikiano mkubwa kwa kutii agizo la serikali kwa kuzingatia bei elekezi jambo ambalo limechangia kulinda maslahi ya wananchi.

PROF. MBARAWA: SERIKALI INAENDA KUKARABATI BANDARI KIGOMA

Image
 Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, tarehe 23 Februari, 2026  katika Ziara yake ya Kanda ya Ziwa ametembelea Bandari ya Musoma,na kusisitiza kuwa Serikali inakwenda kuikarabati ili kuendelea kufungua fursa za kiuchumi Mkoa wa Mara Amesema kuwa Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea na ukarabati na maboresho ya Bandari zote za Maziwa  Makuu zikiwemo za Ziwa Nyasa, Tanganyika na Ziwa Victoria kwa lengo la kuimarisha uchukuzi kwa njia ya maji nchini na kuongeza mapato ya wananchi na Mikoa husika sambamba na kufungua uchumi wa kikanda. Akizungumza baada ya kutembelea Bandari ya Musoma, Mkoani Mara Waziri Mbarawa amesema Ziwa Victoria upande wa mkoa wa Mara ndiyo eneo pekee linalopakana na Nchi mbili za Uganda na Kenya hivyo kuna umuhimu mkubwa wa kufanya maboresho ya Bandari ya Musoma ili kuufungua Mkoa wa Mara na kuiufungua nchi Kikanda Ameeleza kuwa Serikali imeendelea kuwekeza katika miundombinu ya Bandari, ujenzi na ukarabati wa...

WATENDAJI SMZ WATAKIWA KUFUATILIA MWENENDO BEI ZA VYAKULA

Image
                                           Na Mwandishi Wetu, Zanzibar WATENDAJI wenye dhamana katika sekta ya biashara katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), wametakiwa kufuatilia mwenendo wa bei za vyakula katika masoko Unguja na Pemba ili kuwalinda wananchi dhidi ya mfumuko wa bei usio wa lazima. Akizungumza Ofisini kwake Mjini Unguja 23 Februari 2026, Katibu wa Kamati Maalum NEC Zanzibar, Idara ya Itikadi Uenezi na Mafunzo Khàmis Mbeto Khamis alisema kuna bidhaa za vyakula ambavyo serikali ilitoa bei elekezi kabla ya kuanza mfungo wa Ramadhani. Mbeto ambaye karibuni alifanya ziara katika masoko ya Unguja, alisema  baadhi ya bidhaa kama unga wa ngano, mafuta ya kula na zingine bei elekezi ilitolewa hivyo wana wajibu wa kuhakikisha bei hizo rafiki kwa wananchi zinafuatwa. Pia Mwenezi Mbeto amewataka wafanyabiashara kuzingatia maadili na kutopandisha bei za vyakula k...

RAIS DKT. SAMIA, NMB WAMPONGEZA MSHINDI DÀEGU MARATHON 2026

Image
                                            Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam RAIS wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza waTanzania wapenda michezo kumpongeza mwanariadha, Gerald Geay kwa kuwa mshindi wa kwanza, kwa mara ya pili mfululizo, na Emmanuel Dinday kwa kuwa mshindi wa tatu katika Mbio Ndefu za Daegu (Daegu Marathon) 2026 zilizofanyika nchini Korea Kusini.  "Mlijiandaa vizuri, mmejituma kwa bidii na mmestahili ushindi" anaandika Rais  Dkt. Samia kwenye mitandao yake ya kijamii na kuongeza kuwa mafanikio hayo yanaimarisha hadhi yenu ya kimichezo kimataifa, yanaitangaza na kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania. Pia ni funzo na hamasa kwa wanamichezo wengine na timu zetu kufanya vizuri katika mashindano mbalimbali.  Serikali itaendelea kuweka na kuimarisha mazingira yatakayowawezesha kufanya maandalizi mazuri na kuwa washi...

LONGIDO WAASWA KULINDA IKOLOJIA HIFADHI YA JAMII ENDUIMENT

Image
Na Sixmund Begashe, Arusha Wananchi wa Wilaya ya Longido wamezidi kunufaika na matunda ya uhifadhi wa maeneo yaliyohifadhiwa kisheria zikiwemo Hifadhi ya Taifa Arusha na Hifadhi ya Taifa Kilimanjaro (KINAPA). Hayo yameelezwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji kwenye Mkutano wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Lameki Nchemba na wananchi wa Wilaya ya Longido Mkoani Arusha.  Amesema kuwa, kwa mwaka, 2024/2025, Hifadhi ya Jamii ya Wanyamapori ya Enduimet imepokea kiasi cha TShBilioni 1.3, huku Halmashauri ya Wilaya ya Longido imepokea zaidi ya TSh.Milioni 700 kupitia Utalii wa uwindaji na wa picha.                            Waziri Ashatu ameendelea kuwaasa wananchi hao, kuendelea kushirikiana na Wizara hiyo ili kulinda Ikolojia ya Hifadhi hizo dhidi ya uharibifu ukiwemo uingizaji wa mifugo, uchomaji wa moto pamoja na ujangili.

TANZANIA KUSHIRIKI WIKI YA NISHATI ENDELEVU SADC

Image
BALOZI wa Tanzania nchini Zimbabwe, CP Suzana S. Kaganda, akiambatana na Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga, wameongoza ujumbe wa Tanzania kushiriki shughuli ya ukaribisho katika Mkutano wa Wiki ya Nishati Endelevu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaofanyika mjini Victoria Falls, nchini Zimbabwe. Akifungua vikao vya awali vya mkutano huo, Waziri wa Nishati wa Jamhuri ya Zimbabwe, July Moyo, aliwakaribisha washiriki wote na kuwataka kufanya maandalizi madhubuti kuelekea ufunguzi rasmi utakaofanyika 25 Februari 2026. Amesema mkutano huo unafanyika chini ya kaulimbiu isemayo “Kuendeleza Ukuaji wa Uchumi wa Kikanda kupitia Nishati Safi na Matumizi Bora ya Nishati.” Mkutano wa Wiki ya Nishati Endelevu wa SADC unawakutanisha mawaziri na wadau mbalimbali wa sekta ya nishati kutoka nchi wanachama kwa lengo la kujadili na kukuza fursa zilizopo katika nishati endelevu pamoja na programu zinazohusu mnyororo mzima wa thamani wa sekta hiyo. Mkutano huo p...