CCM YAMTEUA DKT. KOMBA UBUNGE PERAMIHO


                                           Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

KAMATI Kuu ya Halmashauri Kuu  ya CCM Taifa imemteua Dkt. Lazaro Kilian Komba kuwa mgombea ubunge  Jimbo la Peramiho katika uchaguzi mdogo  unaotarajiwa kufanyika baadae mwaka huu 2026 kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo, Jenister Mhagama lililopo Wilaya ya Songea  Vijijini, Mkoa wa Ruvuma.

Kikao cha kamati  hiyo kimefanya  uteuzi huo kwa kuzingatia mamlaka iliyopewa chini ya Ibara ya 105 (7)(f) ya Katiba ya CCM  ya Mwaka 1977 toleo la Julai 2025.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyosainiwa na Katibu wa Halmashauri Kuu CCM Taifa (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenan Kiongosi, pia kamati hiyo imewachagua  wagombea  wa  nafasi mbalimbali  bungeni.

"Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu CCM Taifa tarehe 25 Januari 2026 imepitia na kujadili kishja  kufanya uteuzi  wa wagombea uongozi wa CCM wanaotokana na Bunge la Jamhuri  ya Muungano wa  Tanzania" inasema sehemu  ya taarifa hiyo.

Inawataja wajumbe wa Halmashauri Kuu  CCM Taifa wanaotokana na  Bunge toka Bara (nafasi 3) kuwa  ni Paul Makonda na Livingstone Lusinde wakati wanawake (nafasi  1) ni Asia Abdulkarim Halamga.

Wanaotokana  na Bunge Zanzibar (nafasi 2) ambao ni Khamis Mussa Omary na wanawake ni Tauhida Cassian Galos na Katibu wa Wabunge wote (nafasi 1) ameteuliwa Agnes Elias Hokororo.

Wenyeviti wa Bunge (nafasi 3) nao ni Najma Murtaza Giga, Deodatus Philipo Mwanyika, Cecilia Daniel Pareso pia kamati hiyo imefanya uteuzi wa wagombea uongozi CCM wanaotokana na Baraza la Wawakilishi.

Wanaume (nafasi 2) ni pamoja na Said Ali Juma, Hamza Hassan Juma na wanawake (1), Lela Mohammed Mussa.

Wawakilishi wa CCM wanaoingia Bungeni kwa Mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wanaume (nafasi 3), Bakar Hamad Bakari, Dkt. Shahame Ali Ali na Simai Mohamed Said wakati wanawake (nafasi 1), Fatma Ramadhan Mandoba na Katibu wa Wawakilishi wote (nafasi 1), Machano Othmam Said.

Wenyeviti Baraza la Wawakilishi (nafasi 1) ni Mahmoud Omary Hamad na Udhaima Mbarak Tahir.

Comments

Popular posts from this blog

CCM YAISHUKURU SMZ, WAKAZI KIKWAJUNI

CCM YAONYA WATEULE MIUNDOMBINU ZANZIBAR

TRA YATAKIWA IJIPANGE DIRA MAENDELEO YA TAIFA