RAIS DKT. SAMIA MGENI RASMI HARAMBEE UPANDIKIZAJI FIGO, ULOTO
Na Hassan Kimweri, WAF - Dodoma Hospitali ya Benjamin Mkapa imepanga kufanya harambee kwa ajili ya kusaidia matibabu ya upandikizaji Uloto kwa watoto wenye ugonjwa wa Selimundu (sickle cell) na kusaidia matibabu ya upandikizaji Figo kwa wananchi wenye uhitaji,katika kuelekea maadhimisho ya kutimiza miaka 10 ya hospitali hiyo. Kauli hiyo imetolewa 31 Machi 2026 na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa Prof. Abel Makubi,wakati akiongea na wanahabari na waandishi wa habari kuelekea maadhimisho ya miaka kumi ya Hospitali hiyo na kilele chake kimepangwa kufanyike 8 Mei 2026. "Jambo hili tunalifanya Sisi Benjamin Mkapa kwa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), matibabu ya upandikizaji Figo na Uloto yanahitaji gharama kubwa sana, hivyo ni vigumu kwa Mtanzania wa kipato cha chini kumudu gharam...