Posts

Showing posts from April, 2026

RIPOTI YA CAG 2024/2025 YAKABIDHIWA IKULU ZANZIBAR

Image
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameipokea Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Zanzibar (CAG) ya mwaka 2024–2025. Ripoti hiyo imewasilishwa leo, tarehe 30 Aprili 2026, na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Zanzibar, Dkt. Othman Abbas Ali, katika hafla iliyofanyika Ikulu, Zanzibar.

DKT. MWINYI: TUNA KILA SABABU KUENDELEZA USHIRIKIANO NA IRELAND

Image
                                      Na Mwandishi Wetu, Zanziba RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Zanzibar ina kila sababu ya kuendeleza ushirikiano na uhusiano wa muda mrefu baina yake na Ireland. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 30 Aprili 2026, alipokutana na Balozi Nicola Brennan anayeiwakilisha Ireland nchini, aliyefika Ikulu, Zanzibar kwa mazungumzo maalum. _ Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi, akiwa katika mazungumzo na mgeni wake, Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Nicola Brennan, Ikulu Zanzibar. _ Rais Dkt. Mwinyi ameihakikishia Ireland kuwa Zanzibar itaendelea kuendeleza na kuimarisha ushirikiano katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na maendeleo, ustawi wa jamii, biashara na uwekezaji kwa manufaa ya nchi hizo mbili rafiki. Aidha, ameeleza kuwa uhusiano baina ya nchi hizo, ...

DKT. KIJAJI 'ATETA' NA KATIBU MKUU UN-TOURISM

Image
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji, amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Shirika la Utalii la Umoja wa Mataifa (UN Tourism), Shaikha Nasser Al Nowais, tarehe 29 Aprili, 2026 katika eneo la Victoria Falls, ambako ulikuwa unafanyika Mkutano wa Pili wa Kikanda wa UN Tourism kuhusu uwezeshaji wa wanawake katika sekta ya utalii Barani Afrika. Katika mazungumzo hayo, Dkt. Kijaji amempongeza Katibu Mkuu, Al Nowais kwa kuchaguliwa kuwa mwanamke wa kwanza kushika nafasi hiyo, na kusisitiza dhamira ya Tanzania ya kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kimkakati na UN Tourism katika kukuza sekta ya utalii. Aidha, ameangazia mafanikio yaliyopatikana katika sekta hiyo nchini Tanzania na namna yanavyoendelea kuchangia ukuaji wa uchumi. Akizungumzia maandalizi ya AFCON 2027, Dkt. Kijaji ametumia fursa hiyo kumualika rasmi Katibu Mkuu kushiriki na kushuhudia mashindano hayo yatakayofanyika Afrika Mashariki, ikiwemo Tanzania huku akiliomba shirika hilo kuipatia Tanzania msaada ...

RAIS DKT. MWINYI ASHUHUDIA SIMBA IKITWAA KOMBE LA MUUNGANO 2026

Image
  Na Mwandishi Wetu, Zanzibar RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewaongoza maelfu ya mashabiki wa soka kushuhudia mchezo wa fainali wa Ligi ya Muungano kati ya Simba na Yanga, uliochezwa katika Uwanja wa New Amaan Complex, Mkoa wa Mjini Magharibi. Timu ya Simba imefanikiwa kulitwaa kombe la michuano hiyo baada ya kuilaza Yanga 1-0, lililofungwa na mchezaji Selemani Mwalimu katika dakika ya 120 ya mchezo huo uliokuwa mkali na wa kusisimua, kufuatia sare ya bila kufungana katika dakika 90 za kawaida. Rais Dkt. Mwinyi, amelikabidhi kombe la ubingwa huo kwa nahodha wa Simba, Shomari Kapombe, pamoja na Hundi ya TSh. Milioni 150. Pia Rais Dkt. Mwinyi, amekabidhi Hundi yenye thamani ya TSh. Milioni 100 kwa nahodha wa kikosi cha Yanga, Bakari Mwamnyeto, baada ya kuibuka washindi wa pili wa michuano hiyo iliyoandaliwa mahsusi kwa ajili ya maadhimisho ya miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Timu nane zilishiriki michuano hiyo; nn...

RIP MWANAHABARI EDITHA CARLO

Image
 Usiku mbaya kutokana na tasnia  ya habari kumpoteza Mwandishi Editha Carlo aliyekuwa akiripoti kutokea Kigoma. Pumzika rafiki, pumzika mdogo wetu, Poleni sana Kigoma, Mungu awatie nguvu wanafamilia. Mwangwi wa sauti yako ungalipo masikioni mwangu, "Zablon, utakuja lini Kigoma? Njoo kuna stori nyingi sana" mara  ya mwisho miaka kadhaa iliyopita Mtaa wa Samora nikiwa katika 'Kipanya' cha wanahabaÅ•i wa Mwananchi Communicationa Ltd (MCL), tukirejea Tabata kutoka Idara  ya Habari (MAELEZO).

DKT.MWINYI ASHIRIKI KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM TAIFA

Image
MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt.Hussein Ali Mwinyi ameshiriki Kikao cha siku mbili cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM kilichokutana  Jijini Dar es Salaam na kukamilika leo Jumatano tarehe 29 Aprili, 2026. Kikao hicho kimeongozwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan .

DKT. ABBAS: SERIKALI HAIJASIMAMISHA WALA KUZUIA UWINDAJI WA KITALI

Image
                                           Na Anangisye Mwateba-Arusha  SERIKALI imesema haina mpango wa kusimamisha ama kuzuia shughuli za uwindaji wa kitalii na badala yake inaendelea kuandaa na kuboresha sera, sheria na miongozo itakayohakikisha uwindaji wa kitalii unafanyika kwa kuzingatia uhifadhi wa wanyamapori, kukuza mapato ya Taifa na kuchochea maendeleo ya jamii. Akizungumza wakati wa kufungua kikao kazi kati ya Chama cha Wamiliki wa Kampuni za Uwindaji Tanzania ( TAHOA), Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Hassan Abbas alisema, Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inatambua na kuenzi sekta ya wanyamapori kwakuwa ni rasilimali ya kipekee yenye mchango mkubwa katika uchumi wa Taifa, uhifadhi wa mazingira na ustawi wa jamii na hivyo haina mpango wa kuisimamisha bali kuiendeleza.   _ Mwenyekiti wa TAHOA, Michel Manth...

WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA BELARUS ATUA NCHINI, ZIARA YA KIKAZI

Image
                                      Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam WAZIRI wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Belarus, Maxim Ryzhenkov, amewasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia 28 Aprili hadi 30, 2026, kufuatia mwaliko wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  Balozi Mahmoud Thabit Kombo. Mheshimiwa Ryzhenkov amewasili kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam (JNIA) na  alipokewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Ngwaru Maghembe, pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Belarus nchini Dzmitry Krasouski. Katika ziara hiyo, Ryzhenkov anatarajiwa kufanya mazungumzo ya pande mbili na mwenyeji wake, Balozi Mahmoud Thabit Kombo, 28 Aprili 2026, jijini Dar es Salaam pia atakutana na viongozi wengine wa Serikali kwa lengo la kuendeleza na kupanua ushirikiano kati ya nchi hizo mbili. Ziara hiyo...

MKAZO WAWEKWA UZALISHAJI WADHIBITI MAAMBUKIZI VITUO VYA AFYA

Image
                                        Na Cletus Sanga – WAF, Morogoro SERIKALI kwa kushirikiana na Shirika la CIHEB Tanzania kupitia mradi wa Usalama wa Afya Duniani (Global Health Security), imeendelea kujenga mtandao imara wa wataalamu wakufunzi (ToTs) wanaosaidia kudhibiti maambukizi katika vituo vya kutolea huduma za afya. Hayo yamebainishwa leo Aprili 27, 2026, Mkoani Morogoro na Mkuu wa Kitengo cha Kuzuia na Kudhibiti Maambukizi Kitaifa, Dkt. Joseph Hokoro wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha kuandaa orodha ya vifaa muhimu vya Kinga na Udhibiti wa Maambukizi (IPC Catalogue), kukamilisha uchambuzi wa takwimu pamoja na kuongeza viashiria vipya katika mfumo wa DHIS2. Dkt. Hokororo amesema kupitia mradi wa Usalama wa Afya Duniani, hospitali za rufaa za mikoa na wilaya zimeendelea kuwa na wataalamu wenye uwezo wa kusimamia mbinu bora za Kinga na Udhibiti wa Maambukizi bila kutegem...

DKT. NCHIMBI ASISITIZA MSHIKAMANO KITAIFA

Image
                            Na Ofisi ya Makamu wa Rais, Dar es Salaam  MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesisitiza umuhimu wa mshikamano wa Kitaifa ikiwa ni namna muhimu ya kuwaenzi waasisi wa Muungano, Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere na Hayati Abeid Amani Karume. Makamu wa Rais ametoa msisitizo huo, wakati wa Tamasha la Usiku wa Mtanzania ikiwa ni shamrashamra za maadhimisho ya Miaka 62 ya Muungano, lililofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam. Amesema ni msisitizo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa vijana na watanzania kwa ujumla kuhusu kuwa na mshikamano kulinda umoja na amani. Makamu wa Rais amewasihi watanzania kutafakari na kujielekeza katika kujenga mshikamano ni kuhakikisha Muungano unalindwa. Amesisitiza umuhimu wa kuvumiliana katika utoaji wa mawazo,...