MELI YA KWANZA YA KIMATAIFA YASHUSHA SHEHENA YA MAFUTA BANDARI JUMUISHI, MANGAPWANI ZAANZIBAR
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar MELI ya kwanza kubwa ya mafuta ya Kimataifa kutoka Saudi Arabia yenye jumla ya lita Milioni 36 za mafuta ya ndege, petroli na dizeli yamewasili katika Bandari Jumuishi ya Mangapwani, Zanzibar. Kuwasili kwa meli hiyo moja kwa moja toka nje ya nchi, sasa kunaiondolea Zanzibar utegemezi wa mafuta yaliyokuwa yakishushwa bandari ya Tanga na kuletwa na meli ndogo Zanzibar jambo ambalo pia lilikuwa linaiongezea gharama ya uchukuzi Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ). Akizungumza kuhusiana na kuwasili kwa shehena hiyo, Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Nishati na Madini Joseph Kirangi alisema kuwasili kwa meli hiyo na kushusha mafuta moja kwa moja Zanzibar ni kutokana na kuimarika kwa miundombinu ya uhifadhi wa raslimali hiyo muhimu kwa uchumi wa Zanzibar. Alisema hatua hiyo inatokana na dhamira ya dhati ya Rais wa Awamu ya Nane Dkt. Hussein Ali Mwinyi ya kuifanya bandari hiyo kuwa jumuishi kwa bidhaa mbalimbali ikiwemo nishati ya mafuta. Kirangi alisema kitambo Zanzibar...