DKT. MAGEMBE: HAKUNA MGONJWA WA KIPINDUPINDU, CHUKUENI TAHADHARI


                                     Na Hassan Kimweri, WAF - Morogoro

Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Grace Magembe amewataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha ili kujikinga na magonjwa ya mlipuko.

Amewataka wananchi kuepuka uchafuzi wa mazingira, kuwa na matumizi sahihi ya maji safi na salama na unawaji wa mikono. 

Dkt. Magembe ametoa rai hiyo Februari 25, 2026 katika tamko alilolitoa la mwenendo wa magonjwa ya mlipuko na udhibiti wa kipindipindu nchini na takriban mwezi mmoja sasa hakujatokea  mgonjwa wa kipindupindu. 

"Serikali imejipanga kufuatilia na kutoa huduma dhidi ya magonjwa yote ya mlipuko na itaendelea kutoa taarifa mara kwa mara iwapo kutakuwa na mabadiliko katika mwenendo wa maambukizi au endapo kutahitajika kuchukua hatua zaidi," amesema Dkt. Magembe.

Comments

Popular posts from this blog

CCM YAISHUKURU SMZ, WAKAZI KIKWAJUNI

CCM YAONYA WATEULE MIUNDOMBINU ZANZIBAR

TRA YATAKIWA IJIPANGE DIRA MAENDELEO YA TAIFA