KITENGO MAAFA WIZARA AFYA WAKUTANA NA WADAU MOROGORO

Na Mwandishi Wetu, Morogoro

WIZARA ya Afya  kupitia Kitengo cha Dharura na Maafa kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu.    

                           

Wanafanya kikao kazi chenye lengo la kupima matumizi ya rasimu ya Mwongozo wa kutuma Timu ya Wataalam kwa ajili ya kukabiliana na matukio ya dharura na maafa ndani na Nje ya Nchi (Personnel deployment Guideline for Public Health emergencies) na wadau wengine ni wara ya Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa, Mambo ya Ndani, Jeshi la Polisi na Wataalam wengine.

Aidha, Juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali ya awamu ya sita katika kukabiliana na matukio ya dharura na maafa katika jamii ya watanzania zimeungwa mkono na wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la Amref Tanzania na Shirika la Afya Duniani (WHO) ambao kupitia mradi wa Pandemic Fund wamewezesha timu ya  Wataalam kufanya kikao kazi hicho.

Kikao kazi hicho kinatarajiwa kufanyika kwa muda wa siku mbili tarehe 3-4 Juni,2026  Mkoani hapa huku mategemeo makubwa yakiwa ni kutoka na mwongozo utakaowezesha wataalamu kwenda kukabiliana kipindi cha matukio ya dharura  mbalimbali yanayoweza kujitokeza katika jamii ya Watanzania au nchi zingine.

 

Comments

Popular posts from this blog

CCM YAISHUKURU SMZ, WAKAZI KIKWAJUNI

CCM YAONYA WATEULE MIUNDOMBINU ZANZIBAR

TRA YATAKIWA IJIPANGE DIRA MAENDELEO YA TAIFA