USHIRIKIANO TANZANIA, SWEDEN WAJADILIWA
KATIBU Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Sweden nchini, Charlotta Ozaki katika ofisi ndogo za Wizara hiyo jijini Dar es Salaam 11 Mei, 2026.
Mazungumzo hayo yalilenga kujadili namna ya kuimarisha ushirikiano na kukuza diplomasia ya uchumi katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara, usafiri, uwekezaji, elimu na nishati.


Comments
Post a Comment