RAIS DKT. MWINYI ASHIRIKI DUA, ATOA POLE

 


Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amejumuika na waumini wa dini ya Kiislamu katika dua maalum ya kumuombea marehemu Sheikh Abuubakar bin Said Al-Abassy.

Dua hiyo imesomwa jana 02 Mei 2026, katika Ukumbi wa Majid uliopo Kiembe Samaki, Mkoa wa Mjini Magharibi. 


_Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, akitoa mkono wa pole kwa familia ya Nadir Abdullatif Al-Wardi nyumbani kwao Chukwani Buyu, na kuwataka kuwa na subira katika kipindi hiki cha msiba mzito, leo Mei 2, 2026._

Rais Dkt. Mwinyi amemuelezea mwanazuoni huyo kuwa alikuwa mtu mwema, mwenye upendo na aliyewafundisha watu wengi elimu ya dini.

Wakati huo huo, Rais Dkt. Mwinyi ametoa mkono wa pole kwa Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Mhe. Nadir Abdullatif Al-Wardi, pamoja na familia yake kufuatia kifo cha baba yao mzazi aliyefariki nchini India.


_Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, akisalimiana na Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Mhe, Nadir Abdullatif Al-Wardi, alipofika nyumbani kwake Chukwani Buyu kutoa mkono wa pole kufuatia kifo cha baba yake mzazi, jana Mei 2, 2026._

Rais Dkt. Mwinyi alifika nyumbani kwa familia hiyo, Chukwani Buyu, kutoa mkono wa pole na kuwataka kuwa na subira katika kipindi hiki cha msiba mzito.

_Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, akisalimiana na Sheikh Said, mtoto wa marehemu Sheikh Abuubakar bin Said Al-Abassy, alipowasili kushiriki dua maalum ya kumuombea marehemu huyo iliyofanyika katika Ukumbi wa Majid, Kiembe Samaki, Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, jana 2 Mei 2026._


Comments

Popular posts from this blog

CCM YAISHUKURU SMZ, WAKAZI KIKWAJUNI

CCM YAONYA WATEULE MIUNDOMBINU ZANZIBAR

TRA YATAKIWA IJIPANGE DIRA MAENDELEO YA TAIFA