MBETO: NI MAKOSA KUDHANI DEMOKRASIA MAANA YAKE HADI CCM ING'OKE MADARAKANI
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimesema ikiwa tafsiri na maana ya demokrasia kwa upinzani ni kuona CCM ikishindwa Uchaguzi, kupoteza Viti vya Udiwani, Ubunge na Uwakilishi, hiyo si tafsiri wala mantiki sahihi ya neno demokrasia.
Aidha CCM kimeapa hakiwezi kushindwa na vyama vilivyoundwa kuanzia Mwaka 1992, kwa kudhani tayari viwe na nguvu za kukishinda chama kilichoshika madaraka miaka zaidi ya 60.
Matamshi hayo yametamkwa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar, Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Khamis Mbeto Khamis , alipozumgumza na wanahabari, ofisini kwake CCM Kisiwandui Unguja.
Mbeto alisema nguvu za chama chochote cha siasa duniani, ni umri na uimara wa chama hicho raslimaliwatu na fedha, mitaji na vitega uchumi, sera makini, oganaizesheni ilioshamiri na mtandao madhubuti wa kisiasa.
Alisema CCM ni chama kilichojijenga kimtandao kipo kila kona Tanzania, kina rasilimali watu, mitaji na vitega uchumi, ivyo si jambo rahisi kudondoshwa na vyama vilivyoundwa mwaka 1992.
"Ni ajabu kusikia upinzani ukidai kura zake zinaibiwa. Vyama hivyo bado vichanga kisiasa havina ubavu wa kushindana na CCM. Hata timu changa za soka hazihimili mikiki mikiki dhidi ya Simba au Yanga Uwanjani" alisema Mbeto.
Aidha akisema bila kukitaja jina chama chochote cha upinzani, alidai kimeweza kununua jengo jipya la Ofisi zake baada ya kulipwa ruzuku kutoka katika Serikali za CCM huku chama hicho kikijigamba kina uwezo wa kuidondosha CCM.
Alipoulizwa iwapo Serikali za CCM zipo tayari kufanya mabadiliko ya katiba, mifumo ya uchaguzi, kitaasisi na sheria ya Uchaguzi, Mbeto alijibu kuwa kipo tayari ingawaje kusitokane na shindikizo au kwa vitisho
"Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameahidi kabla hajaondoka madarakani mwaka 2030 Tanzania itapata Katiba mpya. Lakini hata ikipatikana Katiba , mabadaliko ya mifumo na sheria, upinzani haujapata na havina uwezo wa kuishinda CCM" alieleza.
Katibu huyo Mwenezi alisema ikiwa neno demokrasia kwa tafsiri ya upinzani hadi pale kishindwe uchaguzi, vyama hivyo vitasubiri kwa miaka mingi kwa kuwa CCM bado kitaendelea kuungwa mkono wananchi na kuongoza dola.
"Nimemsikia Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Othman Masuoud Othmam akidai CCM kimejiweka madarakani. Muulizeni kimejiweka kivipi? Uchaguzi haukuafanyika. Vyama havikushriki Uchaguzi na je, Tume ya Uchaguzi haikumtangaza mshindi ? " Alihoji Mwenezi huyo.
Mbeto alimtaja Mgombea huyo wa Urais Zanzibar kupitia ACT Wazalendo, hajawa na sifa za kumshinda Mgombea Urais wa CCM Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi na cha ajabu amekuwa akisimama na kudai ameibiwa kura.
"Ni kura zipi hizo alizoibiwa Othman. Yeye alikuwa wapi wakati kura zikiibiwa .Ziko wapi na kwanini hakuwakamata walioiba. Kama kuiba Kura jambo rahisi yeye na chama chake walishindwaje kuiba? " alishangaa Mbeto.
Hata hivyo Mwenezi huyo alisema kwa nafasi ya Urais Zanzibar, alimtaja Othman kuwa. Mwanasiasa mpya asiye na umaarufu ndani na nje ya ACT , kwa asili na historia ya Siasa za Zanzibar, si mtu anayetambulika na kukubalika.

Comments
Post a Comment