KAMATI ZA BUNGE JAMHURI YA MUUNGANO TANZANIA, DRC ZAKUTANA


MBUNGE wa Bunge la Kitaifa la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Prof. Willy Buhini ameongoza ujumbe wa wabunge kutoka DRC katika kikao na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Viwanda, Uvuvi, Kilimo na Mifugo.

Pia walifanya mazungumzo na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu.

Viongozi hao wamekutana kuzungumzia namna wanavyoweza kuimarisha na kuongeza ushirikiano baina ya Tanzania na DRC katika sekta mbalimbali ikiwemo viwanda, uvuvi, kilimo na mifugo.

Sekta zingine zilizojadiliwa ni miundombinu ya usafirishaji inayowezesha mwingiliano kati ya mataifa yote mawili.

Buhuni aliambatana pia na Balozi wa Tanzania nchini DRC, Said Mshana na Balozi wa DRC nchini Tanzania, Jean Pierre Massala.

Comments

Popular posts from this blog

CCM YAISHUKURU SMZ, WAKAZI KIKWAJUNI

CCM YAONYA WATEULE MIUNDOMBINU ZANZIBAR

TRA YATAKIWA IJIPANGE DIRA MAENDELEO YA TAIFA