CCM YATAKIWA KUWA NA MIRADI MIKUBWA YA KIUCHUMI


                                            Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema wakati umefika kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa na miradi mikubwa ya kiuchumi kwa kutumia rasilimali zake zilizopo katika maeneo mbalimbali ili kukiimarisha kiuchumi na kuongeza uwezo wake wa kuwatumikia wanachama na wananchi.

Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, 10 Mei 2026, alipozungumza na viongozi na wanachama wa CCM wa Mkoa wa Kusini Unguja katika mkutano maalum wa kutoa shukrani baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2025, hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Dkt. Ali Mohammed Shein, Tunguu, Mkoa wa Kusini Unguja.

Amesema chama kisicho na nguvu za kiuchumi hakiwezi kuwa imara, hivyo CCM inakusudia kuanzisha miradi mikubwa itakayokiingizia mapato ya uhakika.

Rais Dkt. Mwinyi pia, amewasisitiza viongozi na wanachama kutumia maeneo yanayomilikiwa na CCM kuwekeza miradi mikubwa itakayosaidia kuongeza mapato, kuimarisha shughuli za chama na kuboresha maslahi ya watendaji wake.)

Akizungumzia maadili ndani ya chama, Dkt. Mwinyi ametoa rai ya kufufuliwa kwa Kamati za Maadili katika ngazi mbalimbali pamoja na kusisitiza matumizi ya vikao vya kikatiba katika kujadili na kuimarisha nidhamu kwa wanachama.



Comments

Popular posts from this blog

CCM YAISHUKURU SMZ, WAKAZI KIKWAJUNI

CCM YAONYA WATEULE MIUNDOMBINU ZANZIBAR

TRA YATAKIWA IJIPANGE DIRA MAENDELEO YA TAIFA