CARITAS- TANZANIA YAHITIMISHA MAFUNZO USIMAMIZI HATARI ZA MAAFA
SHIRIKA la Misaada la Kanisa Katoliki (CARITAS-Tanzania) leo 19 Mei 2026, limehitimisha mafunzo kwa Wakurugenzi na Wataribu wa Maafa wa CARITAS kutoka majimbo mbalimbali nchini yaliyofanyika katika Ukumbi wa Baraza la Maaskofu Katoliki (TÈC), Kurasini Dar es Salaam, kuhusiana na Usimamizi wa Hatari za Maafa na Namna ya Kupunguza athari zake.
Mafunzo hayo ambayo yameratibiwa na Ofisi ya CARITAS - Taifa na yalifunguliwa rasmi na Kaimu Katibu Mkuu Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Padri Alister Makubi.
Mwezeshaji Mkuu katika mafunzo hayo ni Mtaalam wa Maafa kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma, Dkt. Japhet Ringo




Comments
Post a Comment