MWENGE WA UHURU WATUA MKOA WA KASKAZINI UNGUJA
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
Mwenge wa Uhuru watua Mkoa Kaskazini Unguja ambako pamoja na mambo mengine utazindua uwanja wa michezo jumuishi, uliopo Jimbo la Kijini.
Taarifa ya Mwakilishi wa Kijini, Badria Attai Masoud kupitia mitandao yake ya kijamii imesema kuwa pia Mwenge huo utakagua ujenzi barabara ya Kijini na mirad yenye mchango mkubwa kwa jamii.
Mwenge huo pia utapita Wilaya ya Kaskazini 'B' kabla ya kumalizia Kaskazini 'A' 12 April 2026.
Mwakilishi Atai ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Zanzibar, anasema wana uenzi Mwenge kwa vitendo kwa kufanyakazi kwa bidii, kuilinda amani na kushiriki kikamilifu katika miradi ya maendeleo kwa mustakbari bora wa Taifa.





Comments
Post a Comment