MBETO: VIONGOZI CHADEMA HAWANA HISANI WALA KUMBUKUMBU


                                          Na Mwandishi  Wetu, Zanzibar 

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaja safu ya viongozi wapya  wanaokiongoza  Chadema kwa sasa, wengi kati yao ni  wanaharakati 'Uchwara' na si wanasiasa kwa maana hawana sifa hiyo.

Kauli hiyo ya CCM, imefuatia  kitendo kisicho cha kizalendo cha Chadema  kuandikia barua Umoja wa Afrika (AU) kupinga uteuzi wa Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete  kuwa  Mjumbe  Maalum katika Pembe ya Afrika.

Katibu wa Kamati Maalum ya NEC  Zanzibar, Idara ya Itikadi,  Uenezi na Mafunzo, Komredi Khamis Mbeto  Khamis alisema kitendo hicho kimekitia  aibu Chadema na kuonyesha utovu  wa adabu walio nao.

Mwenezi huyo alisemasafu mpya ya  Viongozi wa Chadema  hawana shukrani wala   kumbukumbu.

Mbeto alisema kama kuna Rais aliyekuwa madarakani, akabeba dhima ya  kuheshimu  utawala  bora wa sheria, demokrasia na kuenzi haki za binadamu hajatokea kama Rais Mstaafu  Dkt. Jakaya   Kikwete.

"Wakati Dkt. Kikwete akiwa madarakani , kulikuwa na uhuru mpana wa vvyombo vya hjabari, ustawi wa demokrasia shirikishi na  watu wameweza kukosoa kadri watakavyo" alisema Mwenezi Mbeto.

Alisema viongozi wa Chadema wameingia  Ikulu   na kufanya majadiliano ya  kiTaifa  wakati  Dkt. Kikwete akiwa Rais hivyo Isingetegemewa viongozi wa  Chadema watamke maneno yasio na Afya wala mantiki.

Katibu huyo  Mwenezi  alisema baadhi ya wana CCM, walimkabili Rais Kikwete, wakimtaka  asiwakaribishe  Chadema Ikulu  kwani wanapotoka hupanda majukwaani na kumtukana bila sababu zozote.

"Utawala wa Rais  Kikwete ulipofungua milango ya demokrasia,  utawala bora, uvumilivu wa kisiasa na  kuanza kusomwa  Ripoti za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)   hadharani" alieleza.

Mbeto alisema, hatua ya Chadema hadi kufikia kuuandikia barua  Umoja wa Afrika wakitaka  kupinga uteuzi wa Dkt.  Kikwete ni zaidi  ya upuuzi uliopitiliza.

"Dunia imeushuhudia Utawala wa Dkt.  Kikwete ulivyoheshimu haki, demokrasia na mijadala ya Bunge kuonyeshwa mubashara kupitia runinga . Wabunge wa Chadema ndio waliompigia makofi Dkt. Kikwete alipongia Bungeni  baada ya kustaafu  kwake Urais" alieleza Mbeto.

Hata hivyo Mwenezi huyo alisema sifa za Dkt. Kikwete Kitaifa, Kikanda  na Kimataifa, utumishi  na uwajibikaji wa  Serikali  yake umevunja rekodi.

Dkt. Kikwete akiwa Ikulu, alisema Mbeto, aliwaalika viongozi kadhaa kuitembelea Tanzania

"Marais  kama  Jim Tao, Xi Jinping wa China, Barack  Obama na Wastaafu wawili wa Marakani   G. W. Bush na Bill Clinton waliitembelea  Tanzania.Kuona na kujua yote   haya hakuhitaji tochi wala kufikia elimu ya juu.

Comments

Popular posts from this blog

CCM YAISHUKURU SMZ, WAKAZI KIKWAJUNI

CCM YAONYA WATEULE MIUNDOMBINU ZANZIBAR

TRA YATAKIWA IJIPANGE DIRA MAENDELEO YA TAIFA