RAIS MWINYI AHIMIZA FIDIA KWA WAKATI WANAOPISHA MRADI


 Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyezi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali Mwinyi leo 02  Januri 2026 ameagiza kulipwa fidia mara moja  kwa watu wote wanaopisha mradi wa barabara za  Ng'imbwa ili mradi  uweze   kukamilika  kwa  wakati.

Akizungumza  wakati  wa  kuweka  jiwe la msingi la ujenzi wa daraja la Uzi Ng’mbwa, Mkoa wa Kusini Unguja pamoja na barabara zake.

Dkt. Mwinyi alisema ameagiza kuchukuliwa hatua madhubuti  kuhakikisha  waliopisha mradi wanalipwa kwa wakati.

Alibainisha kuwa  kuchelewesha fidia  kunasababisha miradi kuchelewa  kukamilika.

Alisema katika  hafla hiyo ambayo ni sehemu ya Shamra Shamra za Mapinduzi za Maadhimisho ya miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwa   wananchi  pia wana wajibu wa  kutoa ushirikiano ili kufanikisha mradi huo wenye  thamani ya TSh.Billioni 36.

Daraja hilo   litakuwa  na  urefu  wa Km 2.2 lina uwezo wa kuhimili  magari yenye  uzito hadi kilo 60  na barabara yenye  urefu wa Km 6.5  na  inatarajiwa  kuondoa changamoto ya  muda mrefu ya usafiri na uchukuzi  kwa   wakazi  wa eneo hilo.

Comments

Popular posts from this blog

CCM YAISHUKURU SMZ, WAKAZI KIKWAJUNI

CCM YAONYA WATEULE MIUNDOMBINU ZANZIBAR

TRA YATAKIWA IJIPANGE DIRA MAENDELEO YA TAIFA