KiNONDONI YAPATA UWANJA WA SOKA WA KÌSASA

    
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

KAMPUNI ya simu za mkononi ya TECNO imekabidhi uwanja mpya wa kisasa wa soka uliojengwa kwa gharama ya TShMilioni 125 kwa manispaaa ya Kinondoni ikiwa ni sehemu  ya Mchango wa Kampuni hiyo kwa  Jamii (CSR), eneo la Minazini Kata ya Makumbusho (maarufu kwa Mapilau), Maanipaa ya Kinondoni, Dar es Salaam.

Uwanja huo umejengwa kufuatia maombi ya uongozi wa kampuni hiyo ambao watautunza pia walipokutana na Meya wa Manispaa Kinondoni Songoro Mnyonge la kutaka eneo kwa ajili ya kujenga  kiwanja kwa ajili ya vijana kufanya mazoezi na utakuwa mali ya manisapaa Kinondoni.

Mchakato wa upatikanaji wake   ulifika mezani kwa Mkurugenzi Manispaa Kinondoni, Hajjat Hanifa Suleiman Hamza ambaye aliwapa uhuru wa kuchagua eneo mojawapo kati ya yale waliyopendekeza manispaa



Meya Songoro aliishukuru TECNO kwa kuunga mkono  jitihda za serikali ya Rais Samia ya kukuza na kuendelezaa vipaji vya soka nchini.

Comments

Popular posts from this blog

CCM YAISHUKURU SMZ, WAKAZI KIKWAJUNI

CCM YAONYA WATEULE MIUNDOMBINU ZANZIBAR

TRA YATAKIWA IJIPANGE DIRA MAENDELEO YA TAIFA