TUME KUTATHIMINI FIDIA MIRADI SMZ


                                           Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, ameunda Tume ya  Watu nane kupitia na kutathmini masuala ya fidia kufuatia utekelezaji miradi  ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) Unguja na Pemba.

Taarifa kwa vyombo vya habari leo 31 Desembaa 2025 na kusainiwa na Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Raqey Mohamed ilisema tume hiyo itakuwa na jukumu la kupitia masuala ya fidia na changamoto zilizojitokeza na kuishauri serikali kuchukua hatua stahiki.

Taarifa hiyo imewataka wananchi kuipa ushirikiano tume hiyo pindi itakapofika maeneo husika kwa ajili ya kupata taarifa stahiki kuhusiana na kazi walizopangiwa.

Tume inaundwa na wabobezi katika fani tofauti ambao ni pamoja na Salim Othman Simba ambaye ni mtumishi wa umma mstaafu na mtaalam wa Uthamini.

Yupo pia  Mussa Kombo Mrisho, Mwanasheria, Ofisi ya Rais Ikulu. Khamis Muhidin Bakari, Mhandisi Viwanja vya Ndege Zanzibar na Fauzia Sindi Hassan Msajili katika Bodi ya Usajili wa Wakandarasi Zanzibar.

Wenginer ni Sabrina Yussuf  Shaaban Mtaalam wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Ikulu Zanzibar, Mwanaidi Seleman Ali, mtaalam wa Sayansi ya Jamii katika Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchimi na Ramadhan Nassoro Mwinyi Mtaalam wa Fedhja na Uwekezaji kutoka Sekta Binafsi na Mzee Abdallah Khatib Mtalaam wa Masuala ya Umma ambaye pia anatoka sekta binafsi.

Comments

Popular posts from this blog

CCM YAISHUKURU SMZ, WAKAZI KIKWAJUNI

CCM YAONYA WATEULE MIUNDOMBINU ZANZIBAR

TRA YATAKIWA IJIPANGE DIRA MAENDELEO YA TAIFA