HBD DKT. MWINYI. DUA, VISOMO VYA WANAMICHEZO KILA KONA




Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

WANAMICHEZO Zanzibar wameandaa dua na  sadaka kwa ajili  ya siku  ya kumbukizi ya kuzaliwa Rais wa Zanzibar  na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein  Ali Mwinyi.

Akizungumza kwa  niaba  ya wanamichezo  wa Zanzibar, mchambuzi wa michezo, Ally Rashid Pizaro alisema dua na sadaka vitafanywa viwanja vya ZBC, Unguja.

"Wanamichezo wanashukuru kwa kazi kubwa aliyofanya  katika sekta ya michezo upande wa miundombinu na kumuombea dua kwa mambo makubwa zaidi anayoenda  kufanya  awamu hii inayofuata" alisema.

Alisema wanamichezo wanamtakia Mwenyezi Mungu azidi azidi kumpa uadilifu na moyo wa kuwatumikia waZanzibari. 

Ujenzi wa Kijiji cha AFCON, viwanja vya michezo jumuishi kila wilaya, ukarabati wa Uwanja wa Amaan ambao sasa ni New Amaan Complex na  Gombani Complex Pemba na vingine  ni sehemu  ya sababu  ya wanamichezo hao kuandaa dua na visomo kila kona, Unguja na Pemba.

Comments

Popular posts from this blog

CCM YAISHUKURU SMZ, WAKAZI KIKWAJUNI

CCM YAONYA WATEULE MIUNDOMBINU ZANZIBAR

TRA YATAKIWA IJIPANGE DIRA MAENDELEO YA TAIFA